10 "Shangilia na ufurahie, ee Binti Sayuni, kwa maana ninakuja, nami nitaishi miongoni mwenu," asema Mwenyezi Mungu. 11 "Mataifa mengi yataunganishwa na Mwenyezi Mungu siku hiyo, nao watakuwa watu wangu. Nitaishi miongoni mwenu, nanyi mtajua kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni amenituma kwenu. 12 Mwenyezi Mungu atairithi Yuda kama fungu lake katika nchi takatifu na atachagua tena Yerusalemu.
Publicidade
Publicidade