Pular para o conteúdo
Publicidade

1 Samweli 2

Ombi la Hana

1 Lk 1:46-55;Flp 4:6;Zab 9:14;13:5;20:5Naye Hana akaomba, akasema,

Moyo wangu wamshangilia BWANA,

Pembe yangu imetukuka katika BWANA,

Kinywa changu kimepanuka juu ya adui zangu;

Kwa kuwa naufurahia wokovu wako;

2 Kut 15:11;Isa 6:3;57:15;Kum 4:35;Zab 73:25Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA;

Kwa maana hakuna yeyote ila wewe,

Wala hakuna mwamba kama Mungu wetu.

3 Mal 3:13Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo;

Majivuno yasitoke vinywani mwenu;

Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa,

Naye huyapima matendo kwa mizani.

4 Pinde zao mashujaa zimevunjika,

Na hao waliojikwaa wamepata nguvu.

5 Lk 1:53;Zab 113:9;Isa 54:1;Gal 4:27Walioshiba wamejikodisha ili kupata chakula,

Lakini waliokuwa na njaa sasa hawana njaa tena.

Naam, huyo aliyekuwa tasa amezaa watoto saba,

lakini aliye na watoto wengi amehuzunika.

6 Kum 32:39;Ayu 5:18;Hos 6:1;Yn 5:25-29;11:25,26;Ufu 1:18BWANA huua, naye hufanya kuwa hai;

Hushusha hadi kuzimu, tena huleta juu.

7 Ayu 1:21;5:11;Zab 102:10;75:7BWANA hufukarisha mtu, na hutajirisha;

Hushusha chini, tena huinua juu.

8 Dan 4:17;Mwa 41:14;1 Sam 15:17;Ayu 36:7;Yak 2:5;Ufu 1:6;3:21;Ebr 1:3Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,

Humpandisha mhitaji kutoka jaani,

Ili awaketishe pamoja na wakuu,

Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu;

Kwa maana nguzo za dunia zina BWANA,

Naye ameuweka ulimwengu juu yake.

9 Zab 91:11;1 Sam 14:6Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake;

Bali waovu watanyamazishwa gizani,

Maana kwa nguvu hakuna atakayeshinda;

10 Zab 96:13Washindanao na BWANA watapondwa kabisa;

Toka mbinguni yeye atawapigia radi;

BWANA ataihukumu dunia yote;

Naye atampa mfalme wake nguvu,

Na kuitukuza pembe ya masihi2:10 Neno hili masihi, kwa Kiebrania, maana yake ni Mtiwa mafuta, au, Mwenye kuwekwa wakfu kwa kutiwa mafuta ili awe mfalme, au kuhani, au nabii. Kwa Kigiriki ni Kristo. wake.

Veja também