Petro ahutubia mkutano
14 Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Yudea, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu. 15 Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana; 16 Yoe 2:28-32lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,
17 Yoe 2:28-32Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu,
nitawamwagia watu wote Roho yangu,
na wana wenu na binti zenu watatabiri;
na vijana wenu wataona maono;
na wazee wenu wataota ndoto.