Pular para o conteúdo
Publicidade

Wimbo ulio Bora 3

Ndoto za mapenzi

1 Zab 4:6;6:6;Isa 26:9 Usiku kitandani nilimtafuta mpendwa wa nafsi yangu,

Nilimtafuta, nisimpate.

2 Nikasema, Haya, niondoke nizunguke mjini,

Katika njia zake na viwanjani,

Nimtafute mpendwa wa nafsi yangu.

Nikamtafuta, nisimpate.

3 Wim 5:7;Isa 21:6-8,11,12 Walinzi wazungukao mjini waliniona;

Je! Mmemwona mpendwa wa nafsi yangu?

4 Mit 8:17;4:13;Rum 8:35,39 Kitambo kidogo tu nilipoachana nao,

Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu;

Nikamshika, nisimwache tena,

Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu,

Chumbani mwake aliyenizaa.

5 Wim 2:7 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu,

Kwa paa na kwa ayala wa porini,

Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha,

Hata yatakapoona vema yenyewe.

Bwana arusi na kundi lake wakaribia

6 Wim 8:5;Yer 2:2 Ni nani huyu apandaye kutoka nyikani,

Mfano wake ni nguzo za moshi;

Afukizwa manemane na ubani,

Na mavumbi ya manukato yote ya mchuuzi?

7 Tazama, ni machela yake Sulemani;

Mashujaa sitini waizunguka,

Wa mashujaa wa Israeli.

8 Wote wameshika upanga,

Wamehitimu kupigana;

Kila mtu anao upanga wake pajani

Kwa hofu ya kamsa za usiku.

9 Mfalme Sulemani alijitengenezea machela

Ya miti ya Lebanoni;

10 Mt 22:37;Yn 13:1,34;Rum 5:8;Efe 3:19;1 Pet 1:7,8 Nguzo zake alizitengeneza za fedha,

Na mgongo wake wa dhahabu,

Kiti chake kimepambwa urujuani,

Gari lake limenakishiwa njumu,

Hiba ya binti za Yerusalemu.

11 Ufu 11:15;Zab 110:3;Isa 62:5 Tokeni, enyi binti za Sayuni,

Mtazameni Mfalme Sulemani,

Amevaa taji alilovikwa na mamaye,

Siku ya posa yake,

Siku ya furaha ya moyo wake.

Veja também