Wimbo wa Sifa wa Mariamu
46 1 Sam 2:1-10Mariamu akasema,
Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu;
48 1 Sam 1:11;Lk 1:25;Zab 113:5,6;Lk 11:27Kwa kuwa ameutazama
Unyonge wa mjakazi wake.
Kwa maana, tazama, tokea sasa
Vizazi vyote wataniita mbarikiwa;
49 Zab 111:9Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu,
Na jina lake ni takatifu.
50 Zab 103:13,17Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi
Kwa hao wanaomcha.
51 Zab 89:10;2 Sam 22:28Amefanya nguvu kwa mkono wake;
Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52 Ayu 5:11;12:19;Zab 147:6;1 Sam 2:7Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi;
Na wanyonge amewainua.
53 1 Sam 2:5;Zab 34:10;107:9Wenye njaa amewashibisha mema,
Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.
54 Isa 41:8;Zab 98:3Amemsaidia Israeli, mtumishi wake;
Ili kukumbuka rehema zake;
55 Mwa 17:7;18:18;22:17;Mik 7:20Kama alivyowaambia baba zetu,
Abrahamu na uzao wake hata milele.