Kuanzishwa kwa Chakula cha Bwana.
22 1 Kor 11:23-25Nao walipokuwa wakila, alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa, akasema, Twaeni; huu ndio mwili wangu. 23 Akatwaa kikombe, akashukuru, akawapa; wakakinywea wote. 24 Kut 24:8;Yer 31:31-34;Zek 9:11Akawaambia, Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi. 25 Amin, nawaambia ninyi, Sitakunywa tena kabisa uzao wa mzabibu, hata siku ile nitakapounywa mpya katika ufalme wa Mungu.