3 Isa 57:15Heri walio maskini wa roho;
Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
4 Isa 61:2;Zab 126:5;Ufu 7:17Heri wenye huzuni;
Maana hao watafarijika.
5 Zab 37:11Heri wenye upole;
Maana hao watairithi nchi.
6 Isa 55:1-2Heri wenye njaa na kiu ya haki;
Maana hao watashibishwa.
7 Yak 2:13Heri wenye rehema;
Maana hao watapata rehema.
8 Zab 24:3-4;51:10;73:1;1 Yoh 3:2,3Heri wenye moyo safi;
Maana hao watamwona Mungu.
9 Ebr 12:4Heri wapatanishi;
Maana hao wataitwa wana wa Mungu.
10 1 Pet 3:14Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki;
Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
11 1 Pet 4:14Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. 12 2 Nya 36:16;Mdo 7:52;Yak 5:10;Ebr 11:33-38Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.