Publicidade

Tito 2

Toa mafundisho mema

1 1 Tim 6:3;2 Tim 1:13 Lakini wewe, nena mambo yanayoambatana na mafundisho mema; 2 1 Tim 5:1 ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika subira. 3 1 Tim 3:11 Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wanaofundisha yaliyo mema; 4 ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; 5 Efe 5:22 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.

6 Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi; 7 1 Tim 4:12;1 Pet 5:3 katika mambo yote ukijionesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionesha usahihi na ustahivu, 8 1 Pet 2:15 na maneno yafaayo yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.

9 Efe 6:5;1 Tim 6:1;1 Pet 2:18 Watumwa na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wakaidi, 10 Tit 1:3 wasiwe wezi; bali wauoneshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mungu aliye Mwokozi wetu katika mambo yote. 11 Maana neema ya Mungu iwaokoao wanadamu wote imefunuliwa; 12 Efe 1:4;1 Yoh 2:16 nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; 13 1 Kor 1:7;Rum 5:2;Flp 3:20 tukilitazamia tumaini lenye baraka na kufunuliwa kwa utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; 14 Kut 19:5;Kum 4:20;7:6;14:2;Zab 130:8;1 Pet 2:9;3:13;Gal 1:4;1 Tim 2:6;Efe 2:10;Eze 37:23 ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wake mwenyewe walio na bidii katika matendo mema.

15 1 Tim 4:12 Nena mambo hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote.

Veja também

Tito
Ver todos os capítulos de Tito
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-