Pular para o conteúdo
Publicidade

1 Mambo ya Nyakati 2

Wana wa Israeli na wazawa wa Yuda

1 Mwa 32:28;35:10;Kut 32:13;Hes 1:5-15;13:4-15;1 Fal 18:31;Mwa 29:32;Kut 1:2 Hawa ndio wana wa Israeli; Reubeni, na Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Zabuloni; 2 Mwa 29:35;38:2,7 na Dani, na Yusufu, na Benyamini, na Naftali, na Gadi, na Asheri.

3 Wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela; ambao hao watatu alizaliwa na binti Shua, Mkanaani. Naye Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mbaya machoni pa BWANA; naye akamwua. 4 Mwa 38:29,30;Mt 1:3 Na Tamari, mkwewe, akamzalia Peresi, na Zera. Wana wote wa Yuda ni watano. 5 Mwa 46:12;Rut 4:18 Wana wa Peresi; Hesroni, na Hamuli. 6 Yos 7:1;1 Fal 4:31 Na wana wa Zera; Zabdi, na Ethani, na Hemani, na Kalkoli, na Darda; hao wote ni watano. 7 1 Nya 4:1;Yos 6:18;7:1 Na wana wa Karmi; Akani, yule aliyewataabisha Israeli, kwa kuchukua kilichowekwa wakfu. 8 Na wana wa Ethani; Azaria.

9 Mt 1:3,4 Tena wana wa Hesroni aliozaliwa; Yerameeli, na Ramu, na Kalebu. 10 Rut 4:19;Mt 1:4;Hes 1:7;2:3 Na Ramu akamzaa Aminadabu; na Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa wana wa Yuda; 11 Rut 4:21;Mt 1:4 na Nashoni akamzaa Salmoni; na Salmoni akamzaa Boazi; 12 na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese; 13 1 Sam 16:6,9 na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama; 14 na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai; 15 na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi; 16 2 Sam 2:18 na dada zao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu. 17 2 Sam 17:25 Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.

18 Basi Kalebu, mwana wa Hesroni, akazaliwa wana na mkewe Azuba, na Yeriothi, na hawa ndio wanawe wa kiume; Yesheri, na Shobabu, na Ardoni. 19 Akafa Azuba, naye Kalebu akamtwaa Efrata, aliyemzalia Huri. 20 Kut 31:2;35:30;2 Nya 1:5 Naye Huri akamzaa Uri; na Uri akamzaa Besaleli. 21 Hes 27:1 Na baadaye Hesroni akamwingilia binti wa Makiri, babaye Gileadi; ambaye alimtwaa alipokuwa na umri wa miaka sitini; naye akamzalia Segubu. 22 Na Segubu akamzaa Yairi, aliyekuwa mwenye miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi. 23 Hes 32:41;Kum 3:14;Yos 13:30 Na Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi, pamoja na Kenathi na miji yake, jumla yote miji sitini. Hao wote ni wana wa Makiri, babaye Gileadi. 24 2 Sam 14:2;1 Nya 4:5;2 Nya 11:6;20:20;Neh 3:5;Yer 6:1;Amo 1:1 Tena, baada ya kufa kwake Hesroni huko Kalebu-Efrata, ndipo Abia, mkewe Hesroni, alipomzalia Ashuri, babaye Teboa.

25 Na wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa Ramu, mzaliwa wa kwanza, na Buna, na Oreni, na Ozemu; kwa Ahiya. 26 Naye Yerameeli alikuwa na mke mwingine, jina lake Atara; yeye alikuwa mamaye Onamu. 27 Na wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, na Yamini, na Ekeri. 28 Na wana wa Onamu walikuwa Shamai, na Yada; na wana wa Shamai; Nadabu, na Abishuri. 29 Na mkewe Abishuri aliitwa jina lake Abihaili; naye akamzalia Abani, na Molidi. 30 Na wana wa Nadabu; Seledi, na Apaimu; lakini Seledi alipokufa hakuwa na watoto. 31 Na wana wa Apaimu; Ishi. Na wana wa Ishi; Sheshani. Na wana wa Sheshani; Alai. 32 Na wana wa Yada, nduguye Shamai; Yetheri, na Yonathani; naye Yetheri alipokufa hakuwa na watoto. 33 Na wana wa Yonathani; Pelethi, na Zaza. Hao ndio wana wa Yerameeli. 34 Basi huyo Sheshani alikuwa hana wana wa kiume, ila binti. Naye Sheshani alikuwa na mtumwa, Mmisri, jina lake akiitwa Yarha. 35 Basi akamwoza binti yake aolewe na Yarha, mtumwa wake; naye akamzalia Atai. 36 1 Nya 11:41 Na Atai akamzaa Nathani; na Nathani akamzaa Zabadi; 37 na Zabadi akamzaa Eflali; na Eflali akamzaa Obedi; 38 na Obedi akamzaa Yehu; na Yehu akamzaa Azaria; 39 na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa 40 na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu; 41 na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.

42 Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni. 43 Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema. 44 Naye Shema akamzaa Rahamu, babaye Yorkeamu; na Rekemu akamzaa Shamai. 45 Na mwana wake Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa babaye Beth-suri. 46 Naye Efa, suria yake Kalebu, alimzaa Harani, na Mosa, na Gazezi; naye Harani akamzaa Gazezi. 47 Na wana wa Yadai; Regemu, na Yothamu, na Geshani, na Peleti, na Efa, na Shaafu. 48 Naye Maaka, suria yake Kalebu, akamzalia Sheberi, na Tirhana. 49 Yos 15:17 Tena akamzaa Shaafu, babaye Madmana; na Sheva babaye Makbena; na babaye Gibea; naye binti Kalebu alikuwa Aksa. 50 Hao walikuwa wana wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrata; Shobali, babaye Kiriath-Yearimu; 51 Salma, babaye Bethlehemu; na Harefu, babaye Beth-gaderi. 52 Naye Shobali, babaye Kiriath-Yearimu, alikuwa na wana; Haroe, na nusu ya Wamenuhothi. 53 Na jamaa za Kiriath-Yearimu; Waithri, na Waputhi, na Washumathi, na Wamishrai; katika hao walitoka Wasorathi, na Waeshtaoli. 54 Na wana wa Salma; Bethlehemu, na Wanetofathi, Atroth-beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi, na Wazori. 55 Mwa 15:19;Hes 24:21,22;Amu 1:16;4:11;1 Sam 15:6;2 Fal 10:15;Yer 35:2 Na jamaa za waandishi waliokaa Yabesi; Watirathi, na Washimeathi, na Wasukathi. Hao ndio Wakeni, waliotoka kwake Hamathi, babaye mbari ya Rekabu.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também