11 Maana neema ya Mungu iwaokoao wanadamu wote imefunuliwa; 12 Efe 1:4;1 Yoh 2:16nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; 13 1 Kor 1:7;Rum 5:2;Flp 3:20tukilitazamia tumaini lenye baraka na kufunuliwa kwa utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; 14 Kut 19:5;Kum 4:20;7:6;14:2;Zab 130:8;1 Pet 2:9;3:13;Gal 1:4;1 Tim 2:6;Efe 2:10;Eze 37:23ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wake mwenyewe walio na bidii katika matendo mema.