Pular para o conteúdo
Publicidade

Agradecimento pela vida

Por Bíblia Online

Agradecer pela vida é reconhecer que cada respiração é dom de Deus. Toda criatura que tem fôlego louve ao Senhor — porque Ele nos formou e nos sustenta com amor.

Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA.

Haleluya.

Sifa kwa kupata msaada wa Mungu

Haleluya.

Ee nafsi yangu, umsifu BWANA.

Nitamsifu BWANA muda ninaoishi,

Nitamwimbia Mungu wangu ningali ni hai.

Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu,

Uliniunga tumboni mwa mama yangu.

Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa

Kwa njia ya ajabu ya kutisha.

Matendo yako ni ya ajabu,

Na nafsi yangu yajua sana,

Mifupa yangu haikusitirika kwako,

Nilipoumbwa kwa siri,

Nilipoungwa kwa ustadi katika pande za chini za nchi;

Macho yako yaliniona kabla sijakamilika;

Kitabuni mwako ziliandikwa zote pia,

Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.

Nitamwimbia BWANA maadamu ninaishi;

Nitamshangilia Mungu wangu nikiwa hai;

Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake;

Maana furaha yangu hutoka kwa BWANA.

Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu;

Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;

Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.

Ingieni malangoni mwake kwa shukrani;

Nyuani mwake kwa kusifu;

Mshukuruni, lihimidini jina lake;

Ee Mungu, jinsi zilivyo na thamani fadhili zako!

Wanadamu huukimbilia uvuli wa mbawa zako.

Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako,

Nawe utawanywesha kutoka mto wa furaha zako.

Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima,

Katika nuru yako tutaona nuru.

Shukrani kwa kuponywa maradhi mabaya

Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua,

Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.

Ee BWANA, Mungu wangu,

Nilikulilia ukaniponya.

Umeniinua nafsi yangu,

Ee BWANA, kutoka kuzimu.

Umenihuisha na kunitoa

Miongoni mwao washukao Shimoni.

Uwezo wa Mungu na haki yake

Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote;

Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu;

Nitafurahi na kukushangilia;

Nitaliimbia sifa jina lako, Wewe Uliye juu.

na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo.

Baraka za kiroho katika Kristo

Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;

Mungu ashukuriwe kwa sababu ya kipawa chake, tusichoweza kukisifu kama ipasavyo.

mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru. Naye alituokoa kutoka kwa nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi.

Ukuu wa Kristo

Naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au milki, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.

Nawe utakula ushibe, utamshukuru BWANA, Mungu wako, kwa nchi nzuri aliyokupa.

Ee BWANA umenitetea katika kisa cha nafsi yangu;

Umeukomboa uhai wangu.

Nilishuka hata pande za chini za milima;

Hiyo nchi ambayo mapingo yake yanafunga hata milele;

Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka humo shimoni,

Ee BWANA, Mungu wangu,

Roho yangu ilipozimia ndani yangu,

Nilimkumbuka BWANA;

Maombi yangu yakakufikia,

Katika hekalu lako takatifu.

Seja o primeiro