Publicidade

Confiança

Por Bíblia Online

A confiança em Deus é âncora da alma em tempos de tempestade. Quem confia no Senhor não será abalado — porque o Deus fiel sustenta, protege e guia os que nele esperam.

Confiança inabalável

Tudo posso naquele que me fortalece. O meu Deus suprirá toda necessidade. Quem confia não será confundido.

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.

Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;

Upendo wa Mungu katika Kristo Yesu

Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani awezaye kutupinga?

wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Hakikisho la ulinzi wa Mungu

Aketiye mahali pa siri pake Aliye Juu

Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

Atasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu,

Mungu wangu nitakayemtumaini.

Kwa Mungu wokovu wangu,

Na utukufu wangu;

Mwamba wa nguvu zangu,

Na kimbilio langu ni kwa Mungu.

Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;

Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake.

Nimemtumaini Mungu, sitaogopa;

Mwenye mwili atanitenda nini?

Fundamento de confiança

Deus não é homem para que minta. Todas as suas promessas são firmes. Confiar em Deus é segurança absoluta.

Mungu si mtu, aseme uongo;

Wala si mwanadamu, ajute;

Iwapo amesema, hatalitenda?

Iwapo amenena, hatalitimiza?

Msiwe na tabia ya kupenda fedha; muwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kamwe, wala sitakuacha.

Hata tunathubutu kusema,

Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa;

Mwanadamu atanitenda nini?

Shika mfano wa mafundisho ya kweli uliyoyasikia kwangu, katika imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.

Askari mwema wa Yesu Kristo

Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.

Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote,

Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

Katika njia zako zote mkiri yeye,

Naye atayanyosha mapito yako.

Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote,

Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

Katika njia zako zote mkiri yeye,

Naye atayanyosha mapito yako.

Mkabidhi BWANA kazi zako,

Na mawazo yako yatakuwa kweli.

Atakayelitafakari neno atapata mema;

Na kila amwaminiye BWANA ana heri.

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego;

Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.

Confiar em todas as coisas

Não pertenço ao mundo — minha cidadania é do céu. A confiança cristã repousa na fidelidade de Deus, não nas circunstâncias.

Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.

Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.

Akasema, Yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.

Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kuliko hao?

Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.

Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA,

Ambaye BWANA ni tumaini lake.

Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji,

Uenezao mizizi yake karibu na mto;

Hautaona hofu wakati wa joto ujapo,

Bali jani lake litakuwa bichi;

Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua,

Wala hautaacha kuzaa matunda.

Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.

Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.

Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.

Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

Kuzipima Roho

Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zipimeni hizo roho, kama zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.

Esperar com confiança

O Senhor está perto de todos os que o invocam. Na espera confiante encontramos descanso e direção divina.

BWANA yuko karibu na wote wamwitao,

Wote wamwitao kwa uaminifu.

Uniwezeshe kusikia fadhili zako asubuhi,

Kwa maana nimekutumaini Wewe.

Unifundishe njia nitakayoiendea,

Kwa maana ninakuinulia nafsi yangu.

Hatauacha mguu wako usogezwe;

Akulindaye hatasinzia;

Umtumaini BWANA ukatende mema,

Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.

Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako

Ulizowawekea wakuchao;

Ulizowatendea wakukimbiliao

Mbele ya wanadamu!

Ni nani niliye naye mbinguni,

Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe.

Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.

Ila na aombe kwa imani, pasipo mashaka yoyote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari linalochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

(Maana twaenenda kwa imani, si kwa kuona.)

Seja o primeiro
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_12-11-46-