Publicidade

Salmos 91

Hakikisho la ulinzi wa Mungu

1 Aketiye mahali pa siri pake Aliye Juu

Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

2 Atasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu,

Mungu wangu nitakayemtumaini.

3 Maana Yeye atakuokoa kutoka kwa mtego wa mwindaji,

Na katika maradhi mabaya.

4 Zab 61:4 Kwa manyoya yake atakufunika,

Chini ya mbawa zake utapata kimbilio;

Uaminifu wake ni ngao na kigao.

5 Ayu 5:19;Mit 3:23;Isa 43:2 Hutaogopa hatari za usiku,

Wala mshale urukao mchana,

6 Wala mapigo yajayo usiku,

Wala maafa yatokeayo adhuhuri,

7 Hata watu elfu wakianguka ubavuni pako.

Naam, watu elfu kumi katika mkono wako wa kulia!

Wewe hutakaribiwa na maafa.

8 Mal 1:5 Ila kwa macho yako utatazama,

Na kuyaona malipo ya wasio haki.

9 Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu;

Umemfanya Aliye Juu kuwa makao yako.

10 Mit 1:33;2 The 3:3;2 Pet 2:9 Mabaya hayatakupata wewe,

Wala tauni haitaikaribia hema yako.

11 Mt 4:6;Lk 4:10 Kwa kuwa atakuagizia malaika wake

Wakulinde katika njia zako zote.Zab 34:7;Mt 4:6;Lk 4:10;Ebr 1:14

12 Ayu 5:23;Zab 37:24;Mt 4:6;Lk 4:11 Mikononi mwao watakuchukua,

Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

13 Lk 10:19 Utawakanyaga simba na nyoka,

Mwanasimba na joka utawakanyaga kwa miguu.

14 Kwa kuwa amekaza kunipenda

Nitamwokoa; na kumweka palipo juu,

Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15 Ayu 22:27;Zab 18:3;Yer 33:3;Zek 13:9;Ebr 5:7;Zab 43:2;1 Sam 2:30 Ataniita nami nitamwitikia;

Nitakuwa pamoja naye taabuni,

Nitamwokoa na kumtukuza;

16 Kwa siku nyingi nitamshibisha,

Nami nitamwonesha wokovu wangu.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-04_23-13-58-