Publicidade

Salmos 128

Nyumba ya mwumini yenye furaha
Wimbo wa kupanda mlima.

1 Heri kila mtu amchaye BWANA,

Aendaye katika njia yake.

2 Taabu ya mikono yako hakika utaila;

Utakuwa heri, na kwako kwema.

3 Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,

Katika nyumba yako.

Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni

Wakiizunguka meza yako.

4 Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA.

5 BWANA akubariki toka Sayuni;

Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;

6 Naam, ukawaone wana wa wanao.

Amani ikae na Israeli.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-