Publicidade

Salmos 99

Sifa kwa utukufu wa Mungu

1 BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka;

Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.

2 BWANA ni mkuu katika Sayuni,

Naye ametukuka juu ya mataifa yote.

3 Na walisifu jina lake kuu litishalo;

Ndiye mtakatifu.

4 Mfalme mkuu upendaye hukumu kwa haki;

Umeiimarisha haki;

Umefanya hukumu na haki katika Israeli.

5 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;

Sujuduni penye kiti cha miguu yake;

Ndiye mtakatifu.

6 Musa na Haruni walikuwa makuhani wake,

Na Samweli pia ni miongoni mwa walioliitia jina lake,

Walimlilia BWANA naye akawaitikia;

7 Akasema nao katika nguzo ya wingu.

Wakashika shuhuda zake na amri aliyowapa.

8 Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;

Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe

Ingawa uliwapatiliza matendo yao.

9 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;

Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu;

Maana BWANA, Mungu wetu, ni mtakatifu.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_18-40-07-