Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 6

Sala ya kuponywa ugonjwa hatari

Kwa mwimbishaji: kwa ala za muziki zenye nyuzi; kulingana na mtindo wa Sheminithi. Zaburi ya Daudi.

1 Zab 38:1 BWANA, usinikemee kwa hasira yako,

Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.

2 Hos 6:1 BWANA, unifadhili, maana ninanyauka;

BWANA, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.

3 Mit 18:14;Mt 26:38 Na nafsi yangu imefadhaika sana;

Na Wewe, BWANA, hadi lini?

4 BWANA urudi, uniopoe nafsi yangu,

Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.

5 Zab 30:9 Maana mautini hapana kumbukumbu lako;

Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?

6 Nimechoka kwa kuugua kwangu;

Kila usiku nakibubujikia kitanda changu;

Nililowesha godoro langu kwa machozi yangu.

7 Macho yangu yameharibika kwa masumbufu,

Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi.

8 Mt 7:23;Lk 13:27 Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu;

Kwa kuwa BWANA ameisikia sauti ya kilio changu.

9 Zab 3:4;31:22;40:1,2 BWANA ameisikia dua yangu;

BWANA atayatakabali maombi yangu.

10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,

Watarudi nyuma, kwa ghafla wataaibika.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também