Sala kwa Mungu wakati wa shida
1 Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki,
Uniokoe kutoka kwa mtu wa hila asiye haki.
2 Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa?
Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?
3 Nitumie nuru yako na kweli yako ziniongoze,
Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata katika maskani yako.
4 Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye
furaha yangu na shangwe yangu;
Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.
5 Nafsi yangu, kwa nini kuinama,
Na kufadhaika ndani yangu?
Umtumaini Mungu;
Maana nitamsifu tena,
Aliye msaada wangu,
Na Mungu wangu.