Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 43

Sala kwa Mungu wakati wa shida

1 Zab 7:8 Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki,

Uniokoe kutoka kwa mtu wa hila asiye haki.

2 Zab 28:7;Isa 26:4 Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa?

Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?

3 Zab 2:6;3:4 Nitumie nuru yako na kweli yako ziniongoze,

Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata katika maskani yako.

4 Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye

furaha yangu na shangwe yangu;

Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.

5 Zab 42:5,11 Nafsi yangu, kwa nini kuinama,

Na kufadhaika ndani yangu?

Umtumaini Mungu;

Maana nitamsifu tena,

Aliye msaada wangu,

Na Mungu wangu.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também