Hakikisho la ulinzi wa Mungu
Kwa mwimbishaji: kwa ala za nyuzi za muziki. Ya Daudi.
1 Ee Mungu, ukisikie kilio changu,
Uyasikilize maombi yangu.
2 Toka mwisho wa nchi nitakulilia ninapozimia moyo,
Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.
3 Kwa maana ulikuwa kimbilio langu,
Ngome yenye nguvu adui asinipate.
4 Nitakaa katika hema yako milele,
Na kupata kimbilio chini ya mbawa zako.
5 Maana Wewe, Mungu, umezisikia nadhiri zangu.
Umewapa urithi wao waliogopao jina lako.
6 Utaziongeza siku za mfalme,
Miaka yake itakuwa kama vizazi vingi.
7 Atakaa mbele za Mungu milele,
Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.
8 Ndivyo nitakavyoliimbia jina lako daima,
Ili niondoe nadhiri zangu kila siku.