Publicidade

Salmos 146

Sifa kwa kupata msaada wa Mungu

1 Haleluya.

Ee nafsi yangu, umsifu BWANA.

2 Nitamsifu BWANA muda ninaoishi,

Nitamwimbia Mungu wangu ningali ni hai.

3 Msiwatumainie wakuu,

Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.

4 Pumzi yake inapomtoka, anarudi katika udongo wake,

Siku iyo hiyo mipango yake hutoweka.

5 Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,

Na tumaini lake ni kwa BWANA, Mungu wake,

6 Aliyezifanya mbingu na nchi,

Bahari na vitu vyote vilivyomo.

Huishika kweli milele,

7 Huwafanyia hukumu walioonewa,

Huwapa wenye njaa chakula;

BWANA hufungua waliofungwa;

8 BWANA huwafumbua macho waliopofuka;

BWANA huwainua walioinama;

BWANA huwapenda wenye haki;

9 BWANA huwahifadhi wageni;

Huwategemeza yatima na mjane;

Bali njia ya wasio haki huiharibu.

10 BWANA atamiliki milele,

Mungu wako, Ee Sayuni, kwa vizazi vyote.

Haleluya.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-15_21-32-39-