Shangwe ya kuishi Sayuni
Ya Wakorahi. Zaburi. Wimbo.
1 Msingi wake upo
Juu ya milima mitakatifu.
2 BWANA ayapenda malango ya Sayuni
Kuliko maskani zote za Yakobo.
3 Mambo makuu yanasemwa kukuhusu,
Ee Mji wa Mungu.
4 Nitataja Rahabu na Babeli
Miongoni mwao wanaonijua.
Tazama Filistia, na Tiro, na Kushi;
Wanasema, Huyu alizaliwa humo.
5 Naam, kuhusu Sayuni yatasemwa,
Huyu na huyu alizaliwa humo.
Na Yeye Aliye Juu
Atauimarisha.
6 BWANA ataweka kumbukumbu, awaandikapo mataifa,
Huyu alizaliwa humo.
7 Waimbao na wachezao ngoma na waseme,
Visima vyangu vyote vimo mwako.