1 Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 Mshukuruni Mungu wa miungu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
4 Yeye peke yake afanya maajabu makuu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
5 Yeye aliyeumba mbingu kwa fahamu zake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
6 Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7 Yeye aliyeumba mianga mikubwa;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8 Jua litawale mchana;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9 Mwezi na nyota zitawale usiku;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
10 Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wao wa kwanza;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11 Akawatoa Waisraeli katikati yao;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12 Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
13 Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
14 Akawavusha Israeli katikati yake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
15 Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
16 Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
17 Yeye aliyewapiga wafalme wakuu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
18 Akawaua wafalme mashuhuri;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
19 Sihoni, mfalme wa Waamori;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
20 Na Ogu, mfalme wa Bashani;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
21 Akaitoa nchi yao iwe urithi;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
22 Urithi wa Israeli mtumishi wake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
23 Aliyetukumbuka katika unyonge wetu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
24 Akatuokoa na watesi wetu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
25 Yeye akipaye kila kiumbe chakula chake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
26 Mshukuruni Mungu wa mbingu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.