Wimbo wa kumtumainia Mungu
Kwa mwimbishaji. Ya Daudi.
1 BWANA ndiye niliyemkimbilia.
Mbona mnaiambia nafsi yangu,
Kimbia kama ndege mlimani kwenu?
2 Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta,
Wanaitia mishale yao katika upote,
Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
3 Kama misingi ikiharibika,
Mwenye haki atafanya nini?
4 BWANA yu katika hekalu lake takatifu.
BWANA ambaye kiti chake kiko mbinguni,
Macho yake yanaangalia;
Kope zake zinawapima wanadamu.
5 BWANA humjaribu mwenye haki;
Bali nafsi yake humchukia asiye haki,
Na mwenye kupenda udhalimu.
6 Awanyeshee wasio haki mitego,
Moto na kiberiti na upepo wa joto
Na viwe fungu la kikombe chao.
7 Kwa kuwa BWANA ni mwenye haki,
Apenda matendo ya haki,
Wanyofu wa moyo watauona uso wake.