Publicidade

Salmos 11

Wimbo wa kumtumainia Mungu
Kwa mwimbishaji. Ya Daudi.

1 BWANA ndiye niliyemkimbilia.

Mbona mnaiambia nafsi yangu,

Kimbia kama ndege mlimani kwenu?

2 Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta,

Wanaitia mishale yao katika upote,

Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.

3 Kama misingi ikiharibika,

Mwenye haki atafanya nini?

4 BWANA yu katika hekalu lake takatifu.

BWANA ambaye kiti chake kiko mbinguni,

Macho yake yanaangalia;

Kope zake zinawapima wanadamu.

5 BWANA humjaribu mwenye haki;

Bali nafsi yake humchukia asiye haki,

Na mwenye kupenda udhalimu.

6 Awanyeshee wasio haki mitego,

Moto na kiberiti na upepo wa joto

Na viwe fungu la kikombe chao.

7 Kwa kuwa BWANA ni mwenye haki,

Apenda matendo ya haki,

Wanyofu wa moyo watauona uso wake.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_18-40-07-