Sala ya ushindi wa kitaifa baada ya kushindwa
Kwa mwimbishaji: kwa kufuata mtindo wa Shushani Eduthi. Utenzi wa Daudi; wa kufundisha; wakati alipopambana na Waaramu. Kutoka Naharaimu na Zoba, na Yoabu alipowaua Waedomi 12,000 katika Bonde la Chumvi alipokuwa akirudi.
1 Ee Mungu, umetutupa na kututawanya,
Umekuwa na hasira, uturudishe tena.
2 Umeitetemesha nchi na kuipasua,
Upaponye palipobomoka, maana inatikisika.
3 Umewaonesha watu wako mazito,
Na kutunywesha mvinyo ya kutuyumbisha.
4 Isa 11:10 Umewapa wakuogopao bendera,
Ili itwekwe kwa ajili ya kweli.
5 Zab 108:6 Ili wapenzi wako waopolewe,
Utuokoe kwa mkono wako wa kulia, utuitikie.
6 Zab 89:35;Mwa 12:6;Yos 13:27 Mungu amenena kwa utakatifu wake,
Nami nikishangilia.
Nitaigawanya Shekemu,
Na kulipima bonde la Sukothi.
7 Kum 33:17;Mwa 49:10 Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu,
Na Efraimu ni kinga ya kichwa changu.
Yuda ni fimbo yangu ya kifalme,
8 Moabu ni bakuli langu la kunawia.
Nitamtupia Edomu kiatu changu,
Na kumpigia Filisti kelele za vita.
9 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye boma?
Ni nani atakayeniongoza hadi Edomu?
10 Zab 44:9 Ee Mungu, si Wewe uliyetutupa?
Wala, Ee Mungu, hutoki na majeshi yetu?
11 Utuletee msaada juu ya mtesi,
Maana wokovu wa binadamu haufai kitu.
12 1 Nya 19:13 Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu,
Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu.