Nchi zote zaitwa kumsifu Mungu
Zaburi ya Shukrani.
1 Mshangilieni BWANA, enyi nchi zote;
2 Mtumikieni BWANA kwa furaha;
Njoni mbele zake mkiimba;
3 Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani;
Nyuani mwake kwa kusifu;
Mshukuruni, lihimidini jina lake;
5 Maana BWANA ni mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake katika vizazi vyote.