Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 111

Sifa kwa maajabu ya Mungu

1 Haleluya.111:1 Haleluya: maana yake ni, Msifuni BWANA.

Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote,

Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano.

2 Ayu 38:1 Matendo ya BWANA ni makuu,

Yafikiriwa sana na wapendezwao nayo.

3 Kazi yake imejaa heshima na adhama,

Na haki yake yadumu milele.

4 Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu;

BWANA ni mwenye fadhili na rehema.

5 Amewapa wamchao chakula;

Atalikumbuka agano lake milele.

6 Amewajulisha watu wake uwezo wa matendo yake,

Kwa kuwapa urithi wa mataifa.

7 Zab 19:7 Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu,

Maagizo yake yote ni amini,

8 Ufu 15:3 Yamethibitika milele na milele,

Yamefanywa kwa uaminifu na haki.

9 Ufu 15:3 Amewapelekea watu wake ukombozi,

Ameamuru agano lake liwe la milele,

Jina lake ni takatifu na la kuogopwa.

10 Kum 4:6;Ayu 28:28;Mit 1:7;9:10;Mhu 12:3 Kumcha BWANA ndio mwanzo wa hekima,

Wote wafanyao hayo wana ufahamu mzuri,

Sifa zake zadumu milele.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também