Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 75

Shukrani kwa wema aliotenda Mungu

Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Usiharibu. Zaburi ya Asafu. Wimbo.

1 Ee Mungu, tunakushukuru.

Tunakushukuru kwa kuwa Jina lako liko karibu;

Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.

2 Nitakapoufikia wakati ulioamriwa,

Mimi nitahukumu hukumu za haki.

3 Ebr 1:3 Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki,

Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.

4 Niliwaambia waliojivuna, Msijivune;

Na wasio haki, Msiiinue pembe.

5 Msiiinue pembe yenu juu,

Wala msinene kwa shingo ya kiburi.

6 Maana siko mashariki wala magharibi,

Wala nyikani itokako heshima.

7 1 Sam 2:7;2 Sam 5:2;Dan 2:21;Lk 1:52 Bali Mungu ndiye ahukumuye;

Humdhili huyu na kumwinua huyu.

8 Ayu 21:20;Yer 25:15;Ufu 14:10 Maana mkononi mwa BWANA mna kikombe,

Na mvinyo yake inatoka povu;

Kumejaa machanganyiko;

Naye huyamimina.

Na sira zake wasio haki wa dunia

Watazifyonza na kuzinywa.

9 Bali mimi nitatangaza matendo yako milele,

Nitamwimbia Mungu wa Yakobo.

10 Nguvu zote za wasio haki nitazimaliza,

Lakini nguvu za mwenye haki nitaziimarisha.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também