Publicidade

Salmos 75

Shukrani kwa wema aliotenda Mungu
Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Usiharibu. Zaburi ya Asafu. Wimbo.

1 Ee Mungu, tunakushukuru.

Tunakushukuru kwa kuwa Jina lako liko karibu;

Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.

2 Nitakapoufikia wakati ulioamriwa,

Mimi nitahukumu hukumu za haki.

3 Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki,

Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.

4 Niliwaambia waliojivuna, Msijivune;

Na wasio haki, Msiiinue pembe.

5 Msiiinue pembe yenu juu,

Wala msinene kwa shingo ya kiburi.

6 Maana siko mashariki wala magharibi,

Wala nyikani itokako heshima.

7 Bali Mungu ndiye ahukumuye;

Humdhili huyu na kumwinua huyu.

8 Maana mkononi mwa BWANA mna kikombe,

Na mvinyo yake inatoka povu;

Kumejaa machanganyiko;

Naye huyamimina.

Na sira zake wasio haki wa dunia

Watazifyonza na kuzinywa.

9 Bali mimi nitatangaza matendo yako milele,

Nitamwimbia Mungu wa Yakobo.

10 Nguvu zote za wasio haki nitazimaliza,

Lakini nguvu za mwenye haki nitaziimarisha.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_18-40-07-