Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 64

Sala ya ulinzi kutoka kwa adui

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu;

Unilinde uhai wangu kutoka kwa hofu ya adui.

2 Zab 143:9 Unifiche mbali na njama za watenda mabaya,

Mbali na mipango ya watu wafanyao maovu;

3 Zab 57:4 Waliounoa ulimi wao kama upanga,

Wanaoyalenga maneno ya uchungu kama mishale,

4 Wapate kumpiga mkamilifu faraghani,

Kwa ghafla humpiga bila kuogopa.

5 Walijifanya hodari katika jambo baya;

Hushauriana juu ya kutega mitego;

Wakisema, Ni nani atakayeiona?

6 Ni nani atambuaye maovu yetu?

Tumepanga njama kwa werevu mwingi,

Maana katika moyo wa mtu na fikira mengi yamefichika.64:6 Maana ya mstari huu si dhahiri kwa Kiebrania.

7 Lakini Mungu atawapiga kwa mshale wake,

Na kuwajeruhi ghafla.

8 Mit 12:13 Kwa ajili ya ulimi wao wataangamizwa;

Wote wawaonao watatetemeka kwa hofu.

Wote wawaonao watatikisa kichwa.

9 Na watu wote wataogopa,

Wataitangaza kazi ya Mungu,

Na kuyafahamu matendo yake.

10 Zab 32:11;Flp 4:4 Mwenye haki atamfurahia BWANA na kumkimbilia,

Na wote wenye moyo wa adili watasifu.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também