Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 98

Sifa kwa mwamuzi wa Dunia

Zaburi.

1 Isa 59:16 Mwimbieni BWANA wimbo mpya,

Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.

Mkono wa kulia,

Na mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu.

2 Isa 52:10;Lk 2:30;Isa 62:2;Rum 3:25;Law 26:45;Kum 4:31;Mik 7:20;Lk 1:54;Isa 49:6;Lk 3:6;Mdo 13:47 BWANA ameufunua wokovu wake,

Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.

3 Amezikumbuka rehema zake,

Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.

Miisho yote ya dunia imeuona

Wokovu wa Mungu wetu.

4 Mshangilieni BWANA, nchi yote,

Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni sifa.

5 Mwimbieni BWANA sifa kwa kinubi,

Kwa kinubi na sauti tamu.

6 Hes 10:10;1 Nya 15:28;2 Nya 29:27 Kwa panda na sauti ya baragumu.

Shangilieni mbele za Mfalme, BWANA.

7 Bahari na ivume na vyote viijazavyo,

Ulimwengu nao wanaokaa ndani yake.

8 Mito na ipige makofi,

Milima na iimbe pamoja kwa furaha.

9 Mbele za BWANA;

Kwa maana anakuja kuihukumu nchi.

Atauhukumu ulimwengu kwa uaminifu,

Na mataifa kwa adili.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também