Sifa kwa ukuu Mwingi wa Mungu
1 Haleluya.
Msifuni Mungu katika patakatifu pake;
Msifuni katika anga la uweza wake.
2 Msifuni kwa matendo yake makuu;
Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu;
Msifuni kwa kinanda na kinubi;
4 Msifuni kwa matari na kucheza;
Msifuni kwa zeze na filimbi;
5 Msifuni kwa matoazi yaliayo;
Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA.
Haleluya.