Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 58

Sala ya kutaka kisasi

Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Usiharibu. Utenzi wa Daudi.

1 Ni kweli, enyi wakuu, mnanena haki?

Enyi wanadamu, mnahukumu kwa adili?

2 Zab 94:20 Sivyo! Mioyoni mwenu mnatenda maovu;

Mikono yenu wenyewe inaeneza udhalimu katika nchi.

3 Zab 51:5 Waovu hupotoka hata kabla ya kuzaliwa kwao;

Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.

4 Zab 140:4 Wana sumu mfano wa sumu ya nyoka;

Wao ni kama fira kiziwi azibaye sikio lake.

5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga,

Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.

6 Ayu 4:10 Ee Mungu, uyavunje meno yao vinywani mwao;

Ee BWANA, uyavunje magego ya wanasimba.

7 Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi;

Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu.

8 Kama konokono ayeyukaye na kutoweka,

Kama mimba iliyoharibika, isiyoliona jua,

9 Mit 10:25 Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba,

Ataipeperusha kama chamchela,

Iliyo mibichi na iliyo moto.

10 Kum 32:42;Ayu 22:19;Zab 18:47;Mit 10:11;Ufu 18:20 Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi;

Ataiosha miguu yake katika damu ya wasio haki.

11 Rum 2:6-11;Ayu 34:11;Mhu 5:8;Yer 32:19;Eze 7:27;Rum 14:12;Ufu 2:23 Na mwanadamu atasema,

Hakika iko thawabu yake mwenye haki.

Hakika yuko Mungu

Anayehukumu katika dunia.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também