Publicidade

Salmos 58

Sala ya kutaka kisasi
Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Usiharibu. Utenzi wa Daudi.

1 Ni kweli, enyi wakuu, mnanena haki?

Enyi wanadamu, mnahukumu kwa adili?

2 Sivyo! Mioyoni mwenu mnatenda maovu;

Mikono yenu wenyewe inaeneza udhalimu katika nchi.

3 Waovu hupotoka hata kabla ya kuzaliwa kwao;

Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.

4 Wana sumu mfano wa sumu ya nyoka;

Wao ni kama fira kiziwi azibaye sikio lake.

5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga,

Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.

6 Ee Mungu, uyavunje meno yao vinywani mwao;

Ee BWANA, uyavunje magego ya wanasimba.

7 Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi;

Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu.

8 Kama konokono ayeyukaye na kutoweka,

Kama mimba iliyoharibika, isiyoliona jua,

9 Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba,

Ataipeperusha kama chamchela,

Iliyo mibichi na iliyo moto.

10 Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi;

Ataiosha miguu yake katika damu ya wasio haki.

11 Na mwanadamu atasema,

Hakika iko thawabu yake mwenye haki.

Hakika yuko Mungu

Anayehukumu katika dunia.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_18-40-07-