Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 76

Mungu wa Waisraeli Mungu mkuu

Kwa mwimbishaji: kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo.

1 Katika Yuda Mungu amejulikana,

Katika Israeli jina lake ni kuu.

2 Kibanda chake pia kiko Salemu,

Na maskani yake iko Sayuni.

3 Zab 46:9;Eze 39:9 Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta,

Ngao, upanga, na zana za vita.

4 Eze 38:12 Wewe U mwenye fahari na adhama,

Toka milima ya mateka.

5 Isa 46:12;Zab 13:3;Yer 51:39 Wametekwa wenye moyo thabiti;

Wamelala usingizi;

Wala hawakuiona mikono yao

Watu wote walio hodari.

6 Kut 15:1;Nah 2:13;Zek 12:4 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo,

Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito.

7 Ayu 41:10;Nah 1:6 Wewe ndiwe utishaye, naam, Wewe;

Naye ni nani awezaye kusimama ukasirikapo?

8 Toka mbinguni ulitangaza hukumu;

Nchi iliogopa, ikakaa kimya.

9 Mungu aliposimama ili kuhukumu

Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia.

10 Kut 9:16 Maana hasira ya binadamu itakusifu,

Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.

11 Mhu 5:4;Zab 68:29 Wekeni nadhiri na mziondoe

Kwa BWANA, Mungu wenu.

Wote wanaomzunguka wamletee hedaya,

Yeye astahiliye kuogopwa.

12 Zab 68:35 Yeye huzikata roho za wakuu;

Na kuwatisha wafalme wa dunia.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também