Utawala wa Mungu juu ya mataifa
Kwa mwimbishaji. Ya Wakorahi. Zaburi.
1 Enyi watu wote, pigeni makofi,
Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.
2 Kwa kuwa BWANA Aliye Juu, mwenye kuogofya,
Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.
3 Amewatiisha watu wa nchi chini yetu,
Na mataifa chini ya miguu yetu.
4 Ametuchagulia urithi wetu,
Fahari ya Yakobo ampendaye.
5 Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
BWANA kwa sauti ya baragumu.
6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa;
Imbeni sifa kwa mfalme wetu, imbeni sifa.
7 Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,
Imbeni kwa zaburi.
8 Mungu ayatawala mataifa,
Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.
9 Wakuu wa watu wamekusanyika,
Kama watu wa Mungu wa Abrahamu.
Maana ngao za dunia zina Mungu,
Ametukuka sana.