Ombi la kupata haki
Zaburi ya Asafu.
1 Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu;
Katikati ya miungu anahukumu.
2 Hadi lini mtahukumu kwa dhuluma,
Na kuzikubali nyuso za wabaya?
3 Mfanyieni hukumu maskini na yatima;
Mtendeeni haki aliyeonewa, na fukara;
4 Mwokoeni maskini na mhitaji;
Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.
5 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani;
Misingi yote ya nchi imetikisika.
6 Mimi nimesema, Ndinyi miungu,
Na wana wa Aliye Juu, enyi nyote.
7 Lakini mtakufa kama wanadamu,
Mtaanguka kama mmoja wa wakuu.
8 Ee Mungu, usimame, uihukumu nchi,
Maana mataifa yote ni yako.