Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 85

Sala ya kupata fadhili za Mungu tena

Kwa mwimbishaji. Ya Wakorahi. Zaburi.

1 Yer 30:18;Eze 39:25 BWANA, umeiridhia nchi yako,

Umewarejesha mateka wa Yakobo.

2 Umeusamehe uovu wa watu wako,

Umezisitiri hatia zao zote.

3 Umeiondoa ghadhabu yako yote,

Umerudi na kuuacha ukali wa hasira yako.

4 Mungu wa wokovu wetu, uturudishe,

Uikomeshe hasira uliyo nayo juu yetu.

5 Je! Utatufanyia hasira hata milele?

Utadumisha ghadhabu kizazi hadi kizazi?

6 Hab 3:2 Je! Hutaki kurudi na kutuhuisha,

Ili watu wako wakufurahie?

7 Ee BWANA, utuoneshe rehema zako,

Utupe wokovu wako.

8 Hab 2:1;Zek 9:10;2 Pet 2:20 Na nisikie atakavyosema Mungu BWANA,

Maana atawaambia watu wake amani,

Naam, na watauwa wake pia,

Bali wasiurudie upumbavu tena.

9 Hakika wokovu wake uko karibu na wamchao,

Ndipo utukufu wake ukae katika nchi yetu.

10 Mik 7:20;Yn 1:17;Zab 72:2,3;Isa 32:17;Lk 2:14;Yn 14:27 Fadhili na kweli zitakutana,

Haki na amani zitakumbatiana.

11 Isa 45:8;2 Kor 5:14-21 Kweli itachipuka katika nchi,

Haki itachungulia kutoka mbinguni.

12 Yak 1:17 Naam, BWANA atatoa kilicho chema,

Na nchi yetu itatoa mazao yake.

13 Haki itakwenda mbele zake,

Na kuzitayarishia hatua zake mapito.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também