Sala ya kushindwa kwa adui za Israeli
Wimbo wa Kupanda mlima
1 Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu,
Israeli na aseme sasa,
2 Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu,
Lakini hawakuniweza.
3 Wakulima wamelima mgongoni mwangu,
Wamefanya mirefu mifuo yao.
4 BWANA ndiye mwenye haki,
Amezikata kamba zao wasio haki.
5 Na waaibishwe, warudishwe nyuma,
Wote wanaoichukia Sayuni.
6 Na wawe kama majani ya darini
Yanyaukayo kabla hayajamea.
7 Ambayo mvunaji haujazi mkono wake,
Wala mfunga miganda kifua chake.
8 Wapitao nao hawasemi, Amani ya BWANA ikae nanyi,
Twawabariki kwa jina la BWANA.