Publicidade

Salmos 114

Maajabu ya Mungu wakati wa kutoka Misri

1 Haleluya.

Israeli alipotoka Misri,

Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.

2 Yuda ilikuwa patakatifu pake,

Israeli milki yake.

3 Bahari iliona ikakimbia,

Yordani ilirudishwa nyuma.

4 Milima iliruka kama kondoo dume,

Vilima kama wana-kondoo.

5 Ee bahari, una nini, ndio ukimbie?

Yordani, ndio urudi nyuma?

6 Enyi milima, ndio mruke kama kondoo dume?

Enyi vilima, kama wana-kondoo?

7 Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana,

Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo.

8 Augeuzaye mwamba kuwa ziwa la maji,

Jiwe gumu kuwa chemchemi.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-18_14-04-22-