Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 114

Maajabu ya Mungu wakati wa kutoka Misri

1 Kut 12:51 Haleluya.

Israeli alipotoka Misri,

Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.

2 Yuda ilikuwa patakatifu pake,

Israeli milki yake.

3 Kut 14:21;Yos 3:16 Bahari iliona ikakimbia,

Yordani ilirudishwa nyuma.

4 Zab 29:6;68:16;Hab 3:6 Milima iliruka kama kondoo dume,

Vilima kama wana-kondoo.

5 Ee bahari, una nini, ndio ukimbie?

Yordani, ndio urudi nyuma?

6 Enyi milima, ndio mruke kama kondoo dume?

Enyi vilima, kama wana-kondoo?

7 Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana,

Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo.

8 Kut 17:1-7;Hes 20:2-13;Zab 107:35 Augeuzaye mwamba kuwa ziwa la maji,

Jiwe gumu kuwa chemchemi.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também