Maajabu ya Mungu wakati wa kutoka Misri
1 Haleluya.
Israeli alipotoka Misri,
Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.
2 Yuda ilikuwa patakatifu pake,
Israeli milki yake.
3 Bahari iliona ikakimbia,
Yordani ilirudishwa nyuma.
4 Milima iliruka kama kondoo dume,
Vilima kama wana-kondoo.
5 Ee bahari, una nini, ndio ukimbie?
Yordani, ndio urudi nyuma?
6 Enyi milima, ndio mruke kama kondoo dume?
Enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana,
Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo.
8 Augeuzaye mwamba kuwa ziwa la maji,
Jiwe gumu kuwa chemchemi.