Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 110

Hakikisho la ushindi kwa mteule wa Mungu

Ya Daudi. Zaburi.

1 Zab 45:6;Mt 22:44;Mk 12:36;Lk 20:42-43;1 Kor 15:25;Mdo 2:34-35;1 Kor 15:25;Efe 1:20-22;Kol 3:1;Ebr 1:13;8:1;10:12-13 Neno la BWANA kwa Bwana wangu,

Uketi upande wangu wa kulia,

Hadi niwafanyapo adui zako

Kuwa chini ya miguu yako.

2 BWANA atainyosha toka Sayuni

Fimbo ya nguvu zako.

Uwe na enzi kati ya adui zako;

3 Amu 5:2;Zab 96:9;Mdo 2:41 Watu wako watajitoa kwa hiari,

Siku ya uwezo wako;

Kwa uzuri wa utakatifu,

Tokea tumbo la asubuhi,

Unao umande wa ujana wako.

4 Hes 23:19;Zek 6:13;Ebr 5:6;6:20;7:17,21 BWANA ameapa,

Wala hataghairi,

Ndiwe kuhani hata milele,

Kwa mfano wa Melkizedeki.

5 Zab 16:8;2:5;Rum 2:5;Ufu 11:18 Bwana yu mkono wako wa kulia;

Atawaponda wafalme,

Siku ya ghadhabu yake.

6 Hab 3:13 Atahukumu kati ya mataifa,

Ataijaza nchi mizoga;

Atawaponda wakuu katika nchi nyingi.

7 Isa 61:1;Yn 3:34;Isa 53:12 Atakunywa maji ya mto njiani;

Kwa hiyo atakiinua kichwa chake kwa ushindi.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também