Hakikisho la ushindi kwa mteule wa Mungu
Ya Daudi. Zaburi.
1 Neno la BWANA kwa Bwana wangu,
Uketi upande wangu wa kulia,
Hadi niwafanyapo adui zako
Kuwa chini ya miguu yako.
2 BWANA atainyosha toka Sayuni
Fimbo ya nguvu zako.
Uwe na enzi kati ya adui zako;
3 Watu wako watajitoa kwa hiari,
Siku ya uwezo wako;
Kwa uzuri wa utakatifu,
Tokea tumbo la asubuhi,
Unao umande wa ujana wako.
4 BWANA ameapa,
Wala hataghairi,
Ndiwe kuhani hata milele,
Kwa mfano wa Melkizedeki.
5 Bwana yu mkono wako wa kulia;
Atawaponda wafalme,
Siku ya ghadhabu yake.
6 Atahukumu kati ya mataifa,
Ataijaza nchi mizoga;
Atawaponda wakuu katika nchi nyingi.
7 Atakunywa maji ya mto njiani;
Kwa hiyo atakiinua kichwa chake kwa ushindi.