Unyonge wa sanamu na ukuu wa Mungu
1 Isa 48:11;Eze 36:32 Ee BWANA, kutukuza usitutukuze sisi,
Bali ulitukuze jina lako,
Kwa ajili ya fadhili zako,
Kwa ajili ya uaminifu wako.
2 Zab 42:3,10;79:10;Yoe 2:17 Kwa nini mataifa kusema,
Yuko wapi Mungu wao?
3 1 Nya 16:26;Zab 135:6;Dan 4:35 Lakini Mungu wetu yuko mbinguni,
Alitakalo lote amelitenda.
4 Kum 4:28;Zab 135:15-18;Isa 40:19;Yer 20:3;Hos 8:6;1 Kor 10:19,20;Ufu 9:20 Sanamu zao ni fedha na dhahabu,
Kazi ya mikono ya wanadamu.
5 Zina vinywa lakini hazisemi,
Zina macho lakini hazioni,
6 Zina masikio lakini hazisikii,
Zina pua lakini hazinusi harufu,
7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi,
Wala hazitoi sauti kwa koo zake.
8 Zab 135:18;Isa 44:9,10;Yon 2:8;Hab 2:18 Wazitengenezao watafanana nazo,
Sawa na wote wanaozitumainia.
9 Zab 33:20;Mit 30:5 Enyi Israeli, mtumainini BWANA;
Yeye ni msaada wao na ngao yao.
10 Mal 2:7 Enyi mlango wa Haruni, mtumainini BWANA;
Yeye ni msaada wao na ngao yao.
11 Enyi mmchao BWANA, mtumainini BWANA;
Yeye ni msaada wao na ngao yao.
12 Efe 1:3 BWANA ametukumbuka,
Naye atatubariki sisi.
Ataubariki mlango wa Israeli,
Ataubariki mlango wa Haruni,
13 Law 26:3;Kum 11:27;Zab 24:4;Mit 10:6;Ufu 11:18;19:5 Atawabariki wamchao BWANA,
Wadogo kwa wakubwa.
14 BWANA na awaongeze ninyi,
Ninyi na watoto wenu.
15 Mwa 14:19;1:1;Zab 96:5 Na mbarikiwe ninyi na BWANA,
Aliyezifanya mbingu na nchi.
16 Mbingu ni mbingu za BWANA,
Bali nchi amewapa wanadamu.
17 Wafu hawamsifu Mungu BWANA,
Wala yeyote ashukaye kwenye kimya;
18 Zab 145:2;Dan 2:20 Bali sisi tutamhimidi BWANA,
Tangu leo na hata milele.