Ombi la huruma
Wimbo wa kupanda mlima.
1 Nimekuinulia macho yangu,
Wewe uketiye mbinguni.
2 Kama vile macho ya watumishi
Yanavyoutegemea mkono wa bwana zao
Kama macho ya mjakazi
Yanavyoutegemea mkono wa bimkubwa wake;
Ndivyo macho yetu yanavyomtegemea BWANA, Mungu wetu,
Hadi atakapoturehemu.
3 Uturehemu, Ee BWANA, uturehemu sisi,
Kwa maana tumeshiba dharau.
4 Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha,
Na dharau ya wenye kiburi.