Sala ya ukombozi kutoka kwa adui
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele?
Hadi lini utanificha uso wako?
2 Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini,
Nikihuzunika moyoni mchana kutwa?
Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini?
3 Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie;
Uyatie nuru macho yangu,
Nisije nikalala usingizi wa mauti.
4 Adui yangu asije akasema, Nimemshinda;
Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.
5 Lakini mimi nimezitumainia fadhili zako;
Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.
6 Naam, nitamwimbia BWANA,
Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.