Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 140

Sala ya ukombozi kutoka kwa adui

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Ee BWANA, uniokoe kutoka kwa watu waovu.

Unihifadhi kutoka kwa watu wajeuri.

2 Waliowaza mabaya mioyoni mwao,

Kila siku huchochea vita.

3 Rum 3:13 Wamenoa ndimi zao na kuwa kama za nyoka,

Na katika midomo yao mna sumu ya fira.

4 Ee BWANA, unilinde Kutoka kwa mikono ya mtu asiye haki;

Unihifadhi na watu wajeuri;

Waliopanga kuniangusha.

5 Zab 10:9;Yer 18:22;Lk 11:53-54 Wenye kiburi wamenifichia mtego na kamba;

Wametandika wavu kando ya njia;

Wameniwekea matanzi.

6 Zab 16:2 Nimemwambia BWANA, Ndiwe Mungu wangu;

Ee BWANA, uisikie sauti ya dua zangu.

7 Kum 33:27-29;Zab 18:32 Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu,

Umenifunika kichwa changu siku ya vita.

8 Ayu 5:12,13 Ee BWANA, usimpe asiye haki tamaa zake,

Usiifanikishe hila yake, wasije wakajiinua.

9 Zab 7:16 Nao wainuapo vichwa watu wanaonizunguka,

Madhara ya midomo yao yawafunike.

10 Zab 11:6 Makaa ya moto yawaangukie, watupwe motoni,

Na katika mashimo, wasipate kusimama tena.

11 Msingiziaji hatawekwa imara katika nchi,

Mtu wa jeuri, uovu humwinda kumwangamiza.

12 Zab 109:31 Najua ya kuwa BWANA atamfanyia mnyonge hukumu,

Na wahitaji haki yao.

13 Hakika wenye haki watalishukuru jina lako,

Wenye adili watakaa mahali ulipo Wewe.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também