Publicidade

Salmos 52

Hukumu kwa waongo
Kwa mwimbishaji. Utenzi wa Daudi, wakati Doegi, Mwedomu alipomwendea Sauli na kumwambia, "Daudi ameingia nyumbani mwa Ahimeleki."

1 Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari?

Wema wa Mungu upo sikuzote.

2 Ulimi wako watunga madhara,

Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila.

3 Umependa mabaya kuliko mema,

Na uongo kuliko kusema kweli.

4 Umependa maneno yote ya kupoteza watu,

Ewe ulimi wenye hila.

5 Lakini Mungu atakuharibu hata milele;

Atakuondolea mbali;

Atakunyakua hemani mwako;

Atakung'oa katika nchi ya walio hai.

6 Nao wenye haki wataona;

Wataingiwa na hofu na kumcheka;

7 Kumbe! Huyu ndiye mtu yule,

Asiyemfanya Mungu kuwa kimbilio lake.

Aliutumainia wingi wa mali zake,

Na kufanya mali kimbilio lake.

8 Bali mimi ni kama mzeituni

Umeao katika nyumba ya Mungu.

Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.

9 Nitakushukuru milele kwa maana umetenda;

Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema;

Mbele ya wacha Mungu wako.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-