Publicidade

Salmos 138

Shukrani na sifa ya Daudi

1 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,

Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.

2 Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu,

Nitalishukuru jina lako,

Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,

Kwa maana umeikuza ahadi yako,

na jina lako juu ya vyote.

3 Siku ile niliyokuita uliniitikia,

Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu.

4 Ee BWANA, wafalme wote wa dunia watakushukuru,

Watakapoyasikia maneno ya kinywa chako.

5 Naam, wataziimba njia za BWANA,

Kwa maana utukufu wa BWANA ni mkuu.

6 Ingawa BWANA yuko juu, anamjali mnyenyekevu,

Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.

7 Nijapopitia katika shida,

Unanilinda juu ya hasira ya adui zangu,

Unaunyosha mkono wako,

Na mkono wako wa kulia unaniokoa.

8 BWANA atanitimizia malengo yake kwangu;

Ee BWANA, fadhili zako ni za milele;

Usiiache kazi ya mikono yako.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-