Mavuno ya shangwe
Wimbo wa kupanda mlima.
1 BWANA alipowarejesha mateka wa Sayuni,
Tulikuwa kama waotao ndoto.
2 Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko,
Na ulimi wetu kelele za furaha.
Ndipo waliposema katika mataifa,
BWANA amewatendea mambo makuu.
3 BWANA alitutendea mambo makuu,
Tulikuwa tukifurahi.
4 Ee BWANA, uwarejeze watu wetu waliofungwa,
Kama vijito vya Kusini.
5 Wapandao kwa machozi
Watavuna kwa kelele za furaha.
6 Ingawa mtu anakwenda zake akilia,
Azichukuapo mbegu za kupanda.
Hakika atarudi kwa kelele za furaha,
Aichukuapo miganda yake.