1 Rehema na hukumu nitaziimba,
Ee BWANA, nitakuimbia zaburi.
2 Nitakuwa na mwenendo usio na hatia;
Utakuja kwangu lini?
Nitakwenda kwa unyofu wa moyo
Ndani ya nyumba yangu.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu
Neno la uovu.
Kazi yao waliopotoka naichukia,
Haitaambatana nami.
4 Moyo wa ukaidi utaondoka kwangu,
Lililo ovu sitalijua.
5 Amsingiziaye jirani yake kwa siri,
Huyo nitamwangamiza.
Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno,
Huyo sitamvumilia.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,
Hao wakae nami.
Yeye aendaye katika njia kamilifu,
Ndiye atakayenitumikia.
7 Hatakaa ndani ya nyumba yangu
Mtu atendaye hila.
Asemaye uongo hatathibitika
Mbele ya macho yangu.
8 Kila asubuhi nitawaangamiza
Waovu wote nchini.
Nikiwatenga wote watendao uovu
Na mji wa BWANA.