Publicidade

Salmos 15

Nani atakaa katika patakatifu pa Mungu?
Zaburi ya Daudi.

1 BWANA, ni nani atakayekaa

Katika hema yako?

Ni nani atakayeishi

Katika kilima chako kitakatifu?

2 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu,

Na kutenda haki.

Asemaye kweli kwa moyo wake,

3 Asiyesingizia kwa ulimi wake.

Wala kumtenda mwenziwe mabaya,

Wala kumsengenya jirani yake.

4 Anayedharau waovu Machoni pake,

Bali huwaheshimu wamchao BWANA

Aliyeapa ingawa kwa hasara yake,

Hayabadili maneno yake.

5 Asiyetoa fedha yake apate kula riba,

Asiyepokea rushwa amwangamize asiye na hatia.

Mtu atendaye mambo hayo

Hataondoshwa milele.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-18_14-04-22-