Kushutumiwa kwa wasiomwamini Mungu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu;
Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo,
Hakuna atendaye mema.
2 Toka mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu,
Aone kama yuko mtu mwenye hekima,
Amtafutaye Mungu.
3 Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja,
Hakuna atendaye mema,
La! Hata mmoja.
4 Je! Wote wafanyao maovu hawajui?
Walao watu wangu kama walavyo mkate,
Hawamwiti BWANA.
5 Hapo ndipo waovu watakaposhikwa na hofu nyingi,
Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.
6 Mnaiharibu mipango ya mtu mnyonge,
Bali BWANA ndiye aliye kimbilio lake.
7 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka katika Sayuni!
BWANA awarudishapo wafungwa wa watu wake;
Yakobo atashangilia,
Israeli atafurahi.