Publicidade

Salmos 23

Mchungaji mwema
Zaburi ya Daudi.

1 BWANA ndiye mchungaji wangu,

Sitapungukiwa na kitu.

2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,

Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza

Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4 Naam, nijapopita kati ya bonde la kivuli cha mauti,

Sitaogopa mabaya;

Kwa maana Wewe upo pamoja nami,

Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

5 Waandaa meza mbele yangu,

Machoni pa watesi wangu.

Umenipaka mafuta kichwani pangu,

Na kikombe changu kinafurika.

6 Hakika wema na fadhili zitanifuata

Siku zote za maisha yangu;

Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-