Deus
Deus é a realidade suprema do universo — o criador, sustentador e redentor de tudo o que existe. Conhecê-lo é a essência da vida eterna e o maior privilégio da existência humana.
Quem é Deus
Não há santo como o Senhor. Tu és grande e fazes maravilhas — só tu és Deus. Sua majestade transcende toda compreensão.
Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA;
Kwa maana hakuna yeyote ila wewe,
Wala hakuna mwamba kama Mungu wetu.
Kwa hiyo, wewe ndiwe mkuu, Ee BWANA Mungu, kwa maana hakuna kama wewe, wala hapana Mungu mwingine ila wewe, kwa kadiri tulivyosikia kwa masikio yetu.
Maana kila nyumba imetengenezwa na mtu; ila yeye aliyevitengeneza vitu vyote ni Mungu.
Ee BWANA, wewe u Mungu wangu;
Nitakutukuza na kulihimidi jina lako;
Kwa kuwa umetenda mambo ya ajabu,
Mashauri ya kale, kwa uaminifu na kweli.
Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA.
Deus é amor
Deus é amor. Quem permanece no amor permanece em Deus e Deus nele. Nós amamos porque Ele nos amou primeiro.
Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.
Sisi tunapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.
Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.
Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.
BWANA, Mungu wako, yuko katikati yako shujaa awezaye kuokoa;
Atakushangilia kwa furaha kuu,
Atakutuliza katika upendo wake,
Atakufurahia kwa kuimba.
Buscar a Deus
Buscareis o Senhor e o encontrareis quando o buscardes de todo o coração. Provai e vede que o Senhor é bom.
Lakini huko, kama mkimtafuta BWANA, Mungu wako, utampata, ukimtafuta kwa moyo wako wote, na roho yako yote.
Onjeni muone ya kuwa BWANA yu mwema;
Heri mtu yule anayemtumainia.
Nimemwambia BWANA, Ndiwe BWANA wangu;
Sina wema ila utokao kwako.
Ni nani niliye naye mbinguni,
Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe.
Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;
Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu;
Kwa ajili ya jina lako uniongoze na unichunge.
Maana yeye anionaye mimi aona uzima,
Naye atapata kibali kwa BWANA.
Viver com Deus
Sê forte e corajoso, porque o Senhor teu Deus é contigo. Em Deus encontramos a razão de existir.
Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja,
Na utukufu wa BWANA umekuzukia.
Kwa maana mimi, BWANA, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kulia, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.
Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.
Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.
Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.