Publicidade

Filhos

Por Bíblia Online

Os filhos são herança do Senhor — bênção e responsabilidade sagrada. A Bíblia orienta sobre a criação dos filhos com amor, disciplina e instrução nos caminhos de Deus.

Herança do Senhor

Os filhos são herança do Senhor e o fruto do ventre é seu galardão. Bem-aventurado o homem que enche deles a sua aljava.

Tazama, watoto ni urithi kutoka kwa BWANA,

Uzao wa tumbo ni thawabu.

Kama mishale mkononi mwa shujaa,

Ndivyo walivyo watoto wa ujanani.

Heri mtu yule

Aliyelijaza podo lake hivyo.

Naam, hawataona aibu

Wanaposema na adui langoni.

Nyumba ya mwumini yenye furaha

Heri kila mtu amchaye BWANA,

Aendaye katika njia yake.

Taabu ya mikono yako hakika utaila;

Utakuwa heri, na kwako kwema.

Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,

Katika nyumba yako.

Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni

Wakiizunguka meza yako.

Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA.

Nyumba ya mwumini yenye furaha

Heri kila mtu amchaye BWANA,

Aendaye katika njia yake.

Taabu ya mikono yako hakika utaila;

Utakuwa heri, na kwako kwema.

Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,

Katika nyumba yako.

Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni

Wakiizunguka meza yako.

Wavulana wetu wakiwa ujanani wawe kama miche

Iliyostawi kikamilifu.

Binti zetu wawe kama nguzo za pembeni

Zilizochongwa ili kupamba kasri.

Wazawa wake watakuwa hodari duniani;

Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.

Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuimiliki; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, kuongezeka kwa ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo wako.

Utabarikiwa kuliko mataifa yote; hakutakuwa na mwanamume wala mwanamke aliye tasa kati yenu; wala kati ya wanyama wenu wa kufugwa.

Instruir e disciplinar

Instrui a criança no caminho em que deve andar, e quando envelhecer não se desviará dele. Disciplina é amor em ação.

Mlee mtoto katika njia impasayo,

Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto;

Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe;

Bali yeye ampendaye humrudi mapema.

Fimbo na maonyo hutia hekima;

Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.

Usimnyime mtoto wako mapigo;

Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

Ushauri wa mzazi

Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu,

Tegeni masikio mpate kujua ufahamu.

Mithali za Sulemani

Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;

Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.

Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyasema uishipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.

O amor de Deus por crianças

Deixai vir a mim as crianças. Jesus acolheu, abençoou e honrou as crianças como modelo de fé e humildade.

Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.

Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu zawadi njema, je! Si Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema zaidi wao wamwombao?

Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake,

Ndivyo BWANA anavyowahurumia wamchao.

Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.

Bênção e promessa

O Senhor te abençoe e te guarde. Os filhos dos justos serão abençoados e suas gerações caminharão na retidão.

BWANA akubariki, na kukulinda;

BWANA akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;

BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.

Mungu na akupe ya umande wa mbingu,

Na manono ya nchi,

Na wingi wa nafaka na mvinyo.

Mataifa na wakutumikie

Na makabila wakusujudie,

Uwe bwana wa ndugu zako,

Na wana wa mama yako na wakusujudie.

Alaaniwe yeyote yule atakayekulaani,

Na abarikiwe yeyote yule atakayekubariki.

Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa; nao watachipua kama nyasi, kama mierebi kandokando mwa vijito.

Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.

Kabla sijakuumba katika tumbo nilikujua, na kabla hujatoka tumboni, nilikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nami nitawapa moyo mmoja na njia moja, wapate kunicha sikuzote; kwa mema yao, na ya watoto wao baada yao;

Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu,

Uliniunga tumboni mwa mama yangu.

Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa

Kwa njia ya ajabu ya kutisha.

Matendo yako ni ya ajabu,

Na nafsi yangu yajua sana,

Mifupa yangu haikusitirika kwako,

Nilipoumbwa kwa siri,

Nilipoungwa kwa ustadi katika pande za chini za nchi;

Macho yako yaliniona kabla sijakamilika;

Kitabuni mwako ziliandikwa zote pia,

Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.

Kwako nilitupwa tangu tumboni,

Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu.

Nilikuwa kijana na sasa ni mzee,

Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa

Wala mzawa wake akiomba chakula.

Mchana kutwa hufadhili na kukopesha,

Na mzao wake hubarikiwa.

Hayo hatutawaficha wana wao,

Huku tukiwaambia kizazi kingine,

Sifa za BWANA, na nguvu zake,

Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.

Wana wa wana ndio taji la wazee,

Na utukufu wa watoto ni baba zao.

Mwenye haki aendaye katika unyofu wake,

Watoto wake wabarikiwa baada yake.

Criação e obediência

Pais, criai vossos filhos na disciplina e instrução do Senhor. Filhos, obedecei a vossos pais — isto é justo e agradável a Deus.

Watoto na wazazi

Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. Waheshimu baba yako na mama yako; hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, Upate heri na kuishi siku nyingi katika dunia.

Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maagizo ya Bwana.

Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.

Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.

Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.

Ni kwa ajili ya kuonywa mnastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyeonywa na babaye? Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali.

Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.

Mwanamke azaapo, ana huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.

Tena, wadogo wenu, mliosema watakuwa mateka, na wana wenu, wasiokuwa leo na maarifa ya mabaya wala mema, ndio watakaoingia, nao ndio nitakaowapa, nao wataimiliki.

Seja o primeiro
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-